Hakika tarehe 26 mach 2011 imeshapita na Tuzo za Kilimanjaro Music Award nazo ndizo zimesha ‘ yeya’, ilikuwa shangwe na furaha na hata wengine kumwaga machozi pindi walipokuwa wakipokea tuzo zao, si hivyo tu, kuna wengine walishindwa hata kujielezea kutokana na furaha waliyokuwa nayo.Tunaweza kusema ni mabadiliko makubwa katika ulimwengu wa sanaa ya muziki wa kizazi kipya hapa nchini, maarufu kama Bongo Fleva. Hii Haijawahi kutokea!! Haijawahi kutokea!! Nimaneno ya mashabiki wa tuzo hizo ambao kwa namna moja au nyingine wameongea maneno hayo wakimaanisha kitu fulani.
Wapo waliosema hivyo wakiamini waliopewa Tuzo ndiyo wasitahiki wa tuzo hizo kupewa, wapo waliosema hivyo kwa kushangaa kwa mwaka huu watu ambao wamezoea kuja kuchukua tuzo wameondoka bila ya tuzo, wapo pia waliosema hivyo kutokana na mtu kupata tuzo nyingi kuliko miaka yoyote ya Tuzo hizi kuanza.
Lakini mwisho wa siku inabaki kuwa watu wote ni kitu kimoja kwakuwa lengo ni kuinua muziki wa Tanzania na si lazima muziki, uchujwe kwa tuzo, ingawa tuzo inaleta hamasha ya kufanya zaidi ya jana na uipite kesho hata kabla haujaifikia.
Wasanii wachanga wameonekana kung’ara zaidi, na wakongwe ndiyo pekee walionekana wakati huu si mzuri kwao, ila wasife moyo ila wajipange kuona jinsi gani wanaweza kuzuia nafasi zao zisizidi kupotea katika tuzo zijazo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, toka THT, Elias Barnaba alkichukua tuzo ya wimbo bora wa Zouk kutoka kwa watangazaji, Dulla wa Channel 5.
Wimbo bora wa RnB, tuzo yake ikakamatwa na Ben Pol akiwa na muda mchache sana kwenye gemu la musiki wa kizazi kipya.
Cpwaa, alijinyakuliwa tuzo mbili, moja ikiwa video bora ya Mwaka
Jcb Pia lipokea tuzo ya muziki bora wa Hi Hop wimbo ‘Ukisikia paaaaaaaaaaaaa’
Jay Mo na Jcb ‘Jacob Makala’ wakipokea tuzo ya wimbo bora wa kushirikiana ‘Ukisikia Paaaaaa “kutoka kwa Monalisa na Ally Rehmtullah
Man Water akipokea miongoni mwa tuzo za Twenty Percent, hii ilitoka kwa mzee wa siku nyingi Kiki.
{gallery}2010/kiliawards2011{/gallery}