Habari
Wasindikaji watakiwa kufuata maelekezo ya TBS na TFDA
Wizara ya viwanda na uwekezaji imewataka wasindikaji kutumia mamlaka zinazohusika na usimamizi wa viwango na ubora ili kuzalisha bidhaa zinazowesha kushindana katika soko la ndani ya nchi na nje.
Akifunga mafunzo ya usindikaji wa chakula jijini Dar es Salaam mwakilishi wa wizara ya viwanda, Boniface Jacob, amesema wasindikaji wanapaswa kufuata maelekezo kutoka shirika la viwango TBS na mamlaka ya chakula na dawa TFDA jinsi ya kuzalisha bidhaa bora zenye viwango.
“Kwahiyo bidhaa kama haijathibitishwa na TBS na kama haijathibishwa na TFDA haiwezi kuuzika kwahiyo haya ni maeneo muhimu sana ni taasisi ambazo zimewekwa kusaidia wajasiliamali kwenye viwanda kwa hiyo mvitumie,”alisema Jacob
BY: EMMY MWAIPOPO