Watafiti wabaini miili ya watu wa kale waliokufa wakiwa wameshikana mikono, masalia hayo yajulikana kama ‘Lovers of Modena’
Watafiti wamebaini kuwa mabaki ya miili ya watu wa kale waliokuwa wameshikana mikono yaliyopatikana Roma , Italia , wote walikuwa wanaume.
Masalio ya mabaki hayo yalijulina kama ‘Lovers of Modena’. Watafiti hawakuweza kugundua jinsia za mabaki hayo wakati walipoyagundua nchini Italia mwaka 2009 kwa sababu walikuwa hawajahifadhiwa vizuri.
Lakini njia mpya ya utafiti wa utafiti wa protini katika meno, umeweza kubainisha jinsia zao.
Uhusiano wa mabaki haya ya watu wa kale ya karne ya 4 mpaka 6 bado haujafahamika. Watafiti wanasema kuwa wanaume hawa walizikwa wakiwa wameshika mikono.Haki miliki ya pichaARCHEOMODEN
Baadhi ya watafiti walihusisha mabaki hayo kwa kudai kuwa walikuwa ndugu au wanajeshi waliokufa pamoja katika vita.
Watafiti hawa wanahusisha vita kwa sababu makaburi mabaki hayo yalipatikana katika makaburi ya vita.Haki miliki ya pichaARCHEOMODENA