Habari
Watu zaidi ya 250 wafariki katika maporomoko nchini Colombia
Watu takribani 254 wamedaiwa kufariki dunia katika maporomoko ya ardhi yaliyotokea katika mji wa Mocoa nchini Colombia baada ya mvua kubwa iliyonyesha Jumamosi.
Vikosi vya uokoaji vinavyoendesha shughuli hiyo vimesema kikwazo kikubwa kwenye zoezi hilo ni barabara nyingi za huko eneo la mji wa kusini mwa mji huo hazipitiki kutokana na kuharibiwa na maporomoko hayo.
Hata hivyo imedaiwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa idadi hiyo kuongezeka kutokana na watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 200 hawajaonekana mpaka sasa.
Rais Juan Manuel Santosa wa nchi hiyo alitangaza hali ya tahadhari katika eneo hilo na kusafiri kuangalia shughuli za uokoaji zinavyoendelea.