Witness kutuwakilisha Nigeria
MC mkali wa Rap anaetamba na wimbo wa ‘Zero’ (Bofya hapa kuangalia Video) , Witness, amechaguliwa
kuwania tuzo za ‘Hip Hop World Awards 2009’ ambazo zitafanyika nchini
Nigeria tarehe 16 Mei.
Witness (wimbo "ZERO") ameingia katika kundi la ‘Msanii Bora wa Afrika (Kutoka nje ya Nigeria), atashindana Buffalo (wimbo "BUBBLE YOUR BUMZ") kutoka Zimbabwe, Tinny (wimbo "I DEY KOLO") kutoka Ghana na Dogg (wimbo "CAN YOU FEEL IT") kutoka Namibia.
Tunamtakia kila la kheri na aendelee kutuwakilisha kama kawaida yake…Bring it home witness!!!