Habari

Wizara ya Afya kuchapisha zabuni zote za Corona – Rais Kenyatta

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameamuru Wizara ya Afya kuchapisha zabuni zote zinazohusiana na jinsi serikali ilivyoshughulikia janga la Covid-19.

Search Results for “mwanasiasa” – Page 8 – Taifa Leo

Zabuni zinazotakiwa kuchapishwa ni zile zilizotolewa na mamlaka ya usambazaji vifaa vya matibabu nchini Kenya (Kemsa).

Amri ya rais inafuatia madai ya ubadhilifu wa fedha za umma uliokumba mchakato wa kutolewa kwa zabuni hizo. Wabunge wameanza uchunguzi binafsi kuhusiana na madai hayo.

Afisa mkuu mtendaji wa Kemsa wiki iliyopita alifahamisha kamati ya bunge la seneti kwamba alipokea maelekezo kutoka kwa Waziri wa Afya Mutahi Kagwe na katibu mkuu katika wizara hiyo Susan Mochache kuhusu jinsi ya kutoa zabuni hizo.

Wawili hao wamesema hawajafanya kosa lolote.

“Wizara ya Afya, katika kipindi cha siku 30 zijazo, lazima ibuni njia mwafaka na iliyo wazi itakayoonesha jinsi Kemsa ilivyotangaza na kupeana zabuni hizo,” Rais Kenyatta alisema hayo siku ya Jumatatu wakati alipoongoza kongamano la magavana kuhusu Covid-19.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents