Michezo

Yaya Toure atajwa tena kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika

Yaya Toure, ametajwa tena miongoni mwa wachezaji watatu bora kuwania taji la mwana soka bora mwaka huu na shirikisho la soka barani Afrika (CAF).

151211161158_yaya_toure_624x351_bbc_nocredit

Tuzo hii huwajumuisha wachezaji wa Afrika wanaocheza soka ng’ambo.

151114103628_andre_ayew_640x360_getty
Andre ‘Dede’ Ayew kutoka Ghana

Nyota huyo wa Manchester City kwa mara nyengine atakuwa akipigania taji hilo dhidi ya mshambulizi wa Black Stars ya Ghana na Swansea Andre ‘Dede’ Ayew na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon na Borussia Dortmund.

24CC6CFA00000578-0-image-a-19_1421529621191
Pierre Emerick Aubameyang kutoka Gabon

Ikiwa atashinda kiungo huyo wa The Elephants ya Ivory Coast Yaya Toure, atakuwa mtu wa kwanza kunyakua taji hilo kwa mara ya tano.

Toure, ambaye aliiongoza Ivory Coast kutwaa ubingwa wa mataifa ya Afrika mapema mwaka huu pamoja na aliyekuwa nahodha wa Cameroon Samuel Eto’o ndio wachezaji wa pekee waliowahi kutwaa taji la mchezaji bora wa Afrika mara 4.

Eto’o alitwaa taji hilo katika miaka ya 2003, 2004, 2005 na 2010.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents