Habari
Zanzibar Update: Boti la Skagit ni mitumba kutoka Marekani
Mtandao wa “The Seattle Times” umeandika kwamba maboti ya Seagull, Skagit na Kalama yaliuzwa Tanzania baada ya kustaafishwa kazi Marekani kwa miaka miwili.
Maboti hayo yalitengenezwa mwaka 1989 na ilipofika hatua ya kuyauza mnunuzi alikosekana kabisa, baada ya kushindwa kuyauza katika mtandao wa eBay akapatikana broker mmoja ambaye aliweza kuyapatia soko nchini kwetu.
Ukweli ni kwamba Tanzania tumezoeshwa mitumba, je historia na uzee wa hiyo boti inaweza kuwa sababu mojawapo ya kuzama kwake leo?
Link ya chanzo chetu hii hapa
http://seattletimes.nwsource.com/html/localnews/2014270612_ferry19m.html