50 Cent anaamini Mayweather atarejea ulingoni
Rapa kutoka nchini Marekani, 50 Cent amesema anaamini siku moja Floyd Mayweather atarejea ulingoni.
Mayweather alistaafu mchezo wa ngumi Septemba mwaka jana baada ya kumpiga mpinzani wake Andre Berto, huku akiwa tayari amefanikiwa kucheza jumla ya mapambano 49 na kufanikiwa kushinda yote na hakuna alilopoteza japo alikuwa anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Manny Pacquiao.
50 Cent ambaye ni rafiki wa karibu wa bondia huyo ameiambia Vanity Fair kuwa kila mpambanaji husema kuwa anastaafu, kwanini aondoke wakati yeye ni mpambanaji mkuwa. Lakini nafikiria atarudi [Myweather] kupambana tena.
“Floyd and I are really good friends, but we argue like regular people argue. The difference is when we have disputes, it winds up on CNN or Instagram. I can cuss him out, call him names, say whatever I want to him, but he’s my little brother,” aliongeza.