Michezo
Pweza awa raia wa Hispania
Pweza wa Ujerumani,almaarufu kama Paul aliyetabiri mechi za kombe la dunia amkiwa ametunikiwa uraia wa Hispania. Pweza Paul amepewa heshima hiyo na mji wa Carbalino baada ya kutabiri kwa usahihi Hispania ingenyakua kombe la dunia. Meya wa mji huo Carlos Montes alikwenda Ujerumani na kukabidhi ngao maalumu iliyo kuwa na maandishi ya kudhibitisha uraia wake.
Alifika katika hifadhi ya viumbe vya baharini ya Oberhausn iliyoko Ujerumani ambako amehifadhiwa Pweza Paul. Alitabiri mechi zote saba ya Ujerumani ikiwamo moja ambayo walifungwa na Hispania.Pweza huyo alitokea kuwa maarufu kwa utabiri wake sahihi wa matokeo baadhi ya fainali za kombe la Dunia.
Sasa ni raia wa Hispania!