Habari
Masoko ya hisa ya US yaanza kudorora kufuatia utabiri wa Trump kuibuka mshindi wa Urais
Masoko ya hisa duniani yameanza kulegalega na yale ya Marekani yakielekea kwenye anguko kubwa kutokana na matokeo ya Urais wa nchi hiyo yanayoendelea kutoka, kuwashangaza wawekezaji duniani.
Donald Trump anaongoza dhidi ya mpinzani wake Hillary Clinton.
Hadi sasa hisa za Dow Jones zimeshuka kwa pointi 800 au 4.4%. Hiyo inalifanya soko la hisa la Marekani kushuka kwa asilimia kubwa tangu August 2011 liliposhuka kwa 5.5%.
Wawekezaji wengi duniani wanaamini kuwa kutotabirika kwa Trump na msimamo wake kibiashara, kutasababisha anguko na hasara kubwa iwapo akishinda.