Kocha wa Klabu ya Simba SC, Pablo Franco amesema idadi ya wachezaji watakao kosekana kwenye mchezo wao dhidi ya Pamba ni kubwa huku akitoa sababu za kukosekana kwao.
Simba SC itashuka dimbani hapo kesho kukabiliana na Klabu ya Pamba hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya Azam Sports Federation Cup.
Inakumbukwa Simba SC haitakuwa na nyota wake Bernard Morrison baada ya kuthibitisha hilo mapema leo mchana ya Mei 13, 2022.