Promotion
John B na Provoke wamleta Cannibal na mixtape yake ‘Prodigal Son’
Watayarishaji wa muziki, John B wa Grandmaster Records ya Arusha na Provoke wa AMG Nairobi, wanamleta mkali kutoka Mombasa, Kenya, Cannibal na mixtape yake, Prodigal Son.
Ni yule yule Cannibal aliyehit na ngoma kama Kichwa Kibovu, I Wish na Legend na collabos kama Badman aliyoifanya na D Knob na My City My Town aliyofanya na Prezzo. Huu ni utangulizi wa albam yake ijayo.
Maproducer hao wameshirikiana na studio zingine kama Mystic,Ufuoni na nyinginezo. Mixtape ina jumla ya nyimbo 19 na kushirikisha stars kama AY,Prezzo,Naziz,Fundi Frank,Abass Kubaff,Bobby Mapesa,Sharama na wengine kibao.
Unaweza kucheck na ngoma zilizopo kwenye prodigal son hapa http://www.mdundo.com/a/44 pia unawezasikiliza preview/kionjo cha mixtape hiyo hapo chini.