Jahazi yafunika bovu sikukuu ya Eid Dar Live chini ya Vodacom Tanzania
Hakika Mzee Yusuph ni mfalme katika muziki wa taarabu maneno hayo yamedhihirika jana usiku, katika viwanja vya Dar Live –Mbagala baada ya kudondosha bonge la shoo, babu kubwa chini ya udhamini wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania pamoja na Global Publishers. Shoo nzima ilihudhuriwa na watu kibao, kiasi kwamba mashabiki walikosa sehemu ya kukaa na kuwabidi kucheza mwanzo mwisho.
Umati wa mashabiki wa muziki wa Taarabu ulivyofurika katika ukumbi wa Dar Live jana kwenye Tamasha la sikukuu ya Eid liliodhaminiwa na Vodacom Tanzania
Mzee Yusuph akiwa na wachezaji wake katika kuwaburudisha wapenzi wa taarabu hapo jana katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania
Baadhi ya waimbaji wa kundi la Jahazi Modern Taarabu wakiwa jukwaani katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania
Mzee Yusuph akiwa kashika fedha alizotunzwa na mashabiki baada ya kukunwa na tungo zake katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania , kushoto ni mcheza shoo wake
Mfalme Mzee Yusuph akiwapa burudani mashabiki waliofurika katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania
Umati wa watu wakiserebuka vilivyo na mirindimo ya Pwani toka kwa Mzee Yusuph katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania
Mfalme Mzee Yusuph akiwa na wacheza shoo wake katika ukumbi wa Dar Live mbagala kwenye tamasha maalum la sikukuu ya Eid lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania