Alikiba aamsha mzuka wa mashabiki wake baada ya kutangaza ujio wa ngoma mpya
Msanii wa muziki, Alikiba ametangaza rasmi ujio wake mpya baada ya ukimya wa muda mrefu hasa hasa baada ya kujiingiza kwenye michezo.
Muimbaji huyo ametangaza kwamba ataachia wimbo ‘Hela’ hatua ambayo imeamsha hisia kwa mashabiki wake ambao walikuwa wanamsubiria kwa hamu.
Kiba ambaye kwa sasa ni mmoja kati ya wadhamini wa timu ya Coastal Union kutoka Tanga inayoshiriki ligu Kuu ya soka Tanzania Bara (TPL), ameonekana kutumia muda wake mwingi kwenye soka kuliko kwenye muziki ambao umemtambulisha.
Mashabiki wengi kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kufurahishwa na kitendo hicho huku wengine wakitaka muimbaji huyo kuachia kazi hiyo mara moja.
Hata hivyo muimbaji huyo hajaweka wazi ni lini ataachia kazi hiyo inayosubiriwa kwa hamu ya mashabiki wa muziki.
Soma maoni ya mashabiki hao.
Rich_kiba
Team Kiba turn on post notification kwenye YouTube ac ya kingkibaa.
Raygunmaterial
YeeehBaba, na wananchi wanalalamika, unapendelea wanasiasa helaaa, @officialalikiba