Burudani
Muda wangu bado, kila kitu kinahitaji subira – Amini
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Amini Mwinyimkuu ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo “Hawajui” amefunguka kwa kusema hafikirii kama anabaniwa na wadau kwenye muziki muziki wa Bongo kama ambavyo imekuwa ikisemwa mara kwa mara.
Akiongea katika kipindi cha Hatua Tatu cha Times Fm ijumaa iliyopita, Amini alisema:
Mwaka 2013 nilifanikiwa kupata tuzo basi unaambiwa wasanii wote walishangilia na kupanda juu ya meza, nafikiri muda wangu bado kila kitu kinahitaji subira, ipo siku tu ntatoa wimbo ambao dunia nzima itaelewa nini nafanya.”
Amini pia ameweka bayana kuwa haamini kama mwanamuziki ukioa ndio tiketi ya kupotea kwenye muziki kama wengi wanavyodai.