Habari

Apigwa faini kwa kumkashifu mkongwe wa vita vya pili vya dunia 

Mahakma nchini Urusi imetoa uamuzi wa kesi ya pili iliyokuwa ikimkabili kiongozi wa upinzani Alexei Navalny.

Image result for Alexei Navalny

Navalny, alipatikana na hatia ya kumkashifu mkongwe mmoja aliyeshiriki kwenye vita vya pili vya dunia na hivyo ametakiwa kulipa faini ya karibu Euro 9,500.

Kabla ya hapo, mahakama ilitupilia mbali rufaa ya kesi yake nyingine aliyowasilisha kupinga umauzi wa kumfunga jela miaka mitatu kwa kosa la kukiuka dhamana.

Wafuasi wake wanadai kuwa mashtaka yote mawili ni njama ya kisiasa ambapo serikali inataka kuunyamazisha upinzani dhidi ya rais wa Urusi Vladimir Putin.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents