Arsenal yalazimishwa sare, yazidi kupeta michuano ya Europa
Klabu ya Arsenal hapo jana usiku ikiwa katika Uwanja wa nyumbani Emirates imekubali kutoka sare ya 0-0 dhidi ya timu ya Red Star Belgrade katika mchezo wa kufuzu hatua ya 32 ya michuano ya Europa League.
The Gunners imefuzu hatua hiyo licha ya kutoka sare ya bila kufungana na Red Star baada ya kuongoza msimamo wa kundi H kwa jumla ya pointi 10 huku timu inayomfuata kwa karibu ya CZvezda ikiwa na alama 5 pekee.
Vikosi vya pande zote mbili
Kwaupande wa Arsenal wachezaji waliyocheza Macey (8), Nelson (7), Debuchy (6), Elneny (6), Holding (6), Maitland-Niles (6), Coquelin (6), Willock (7), Walcott (5), Wilshere (6), Giroud (6).
Mchezaji wa akiba: Nketiah (6)
Upande wa Red Star Belgrade: Borjan (7), Stojkovic (7), Le Tallec (8), Savic (8), Gobeljic (7), Krsticic (6), Donald (6), Srnic (8), Kanga (7), Radonjic (7), Boakye (6).
Wachezaji waakiba: Racic (5), Milic (5), Pesic (5).
Mchezaji bora wa mchezo huo alikuwa: Matt Macey.
Arsenal sasa inarejea katika ligi kuu Uingereza Jumapili kukipiga na Manchester City.