Akaunti ya Twitter ya Rais Donald Trump yapotea hewani kwa muda
Akaunti ya Rais wa Marekani, Donald Trump ya mtandao wa Twitter ilipotea kwa muda wa dakika 11 hewani na kisha kurejea tena hewani baada ya makosa kurekebishwa na mtandao huo.
Twitter wamethibitisha kwa kueleza kuwa kulitoa tatizo la kibinadamu kwenye kampuni yao ambapo moja ya mfanyakazi wao aliisitisha kwa muda (Deactivated) akaunti ya Trump lakini baadae wakagundua tatizo hilo na kuirudisha hewani.
Earlier today @realdonaldtrump’s account was inadvertently deactivated due to human error by a Twitter employee. The account was down for 11 minutes, and has since been restored. We are continuing to investigate and are taking steps to prevent this from happening again.
— Government (@Gov) November 3, 2017
Twitter wameeleza kuwa mfanyakazi huyo aliifuta kimakosa kipindi akijiandaa kuondoka jana usiku lakini wataendelea na uchunguzi zaidi juu ya tukio hilo.
Through our investigation we have learned that this was done by a Twitter customer support employee who did this on the employee’s last day. We are conducting a full internal review. https://t.co/mlarOgiaRF
— Government (@Gov) November 3, 2017
Kitendo hicho cha kupotea kwa muda akaunti hiyo kimewafurahisha baadhi ya watu wanaopinga misimamo na itikadi zake za kiutawala.
Hata hivyo tayari ukurasa huo wa Rais ,Donald Trump (@RealDonaldTrump) umerejea hewani na mwenyewe hajazungumzia chochote mpaka sasa hivi.