Habari
Atimuliwa kwenye fainali ya mechi ya darts kwa kufanana na ‘Yesu’
Shabiki wa DARTS huko nchini Uingereza amelazimika kuondoka nje ya fainali ya mechi ya mchezo huo uliokuwa ukirushwa live kwa kufanana na Yesu.
Nathan Grindal mwenye ndevu, 33, alikuwa akifurahia mechi kati ya nyota Phil Taylor na Kim Huybrechts ndipo umati wa watu 4,500 ulipoanza kumzomea kwa kufanana na mwana wa Mungu.
Baada ya fujo kuwa kubwa mabaunsa sita walimtoa nje Nathan.
http://www.youtube.com/watch?v=80dlTWn9mpw
Umati huo ulikuwa ukipiga mayowe ukisema ‘simama kama unampenda Yesu’