Burudani

Big Sean amchimba mkwara Justin Bieber baada ya ‘kumbambia’ girlfriend wake Ariana Grande jukwaani

Muimbaji Justin Bieber amemfanya rapper Big Sean kupata wivu na wasiwasi kuwa huenda akaibiwa tunda lake, baada ya muimbaji huyo wa Canada kumkumbatia girlfriend wa rapper huyo Ariana Grande jukwaani.

Ariana & Justin

Ariana alikua akitumbuiza huko Los Angeles, Marekani Jumatano wiki hii na Bieber alipanda jukwaani kama ‘surprise’ na kutumbuiza naye.

Ariana & Justin4

Wakiwa wanaimba pamoja Bieber alimkumbatia na kumshika kimahaba Ariana kama couple, kiasi cha kumfanya Big Sean apatwe na wivu na kushindwa kuvumilia. Inasemekana kuwa Sean alitumia Twitter kumchimba mkwara Bieber kwa kuandika, “huyu mtoto anatakiwa ajifunze kutomshika hivyo msichana wangu”, tweet ambayo inaaminika baadaye ilifutwa.

Big Sean tweet

Hata hivyo vyanzo vingine viliuambia mtandao wa TMZ kuwa tweet hiyo ilikuwa feki.

Ariana & Justin2

Ariana & Justin3

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents