Burudani

Cassim Mganga kufanyia video ya ‘Subira’ Tanga

Cassim Mganga ambaye kwa sasa anafanya vyema na wimbo wake ‘Subira’ aliomshirikisha Christian Bella, amesema video ya wimbo huo itafanyika Tanga.

caa

Akiongea na E-News ya EATV, Cassim alidai kuwa awali alipanga kwenda kuifanyia nje ya nchi lakini amebadilisha mawazo na kuamua kwenda kule mapenzi yalikozaliwa!

“Video tunafanya mwezi huu na Mungu akipenda nitaiachia mwezi huu mwishoni na itafanyika Tanga,” alisema.

“Mwanzo tulikuwa na presha ya kwenda kuifanya nje ya nchi lakini baadaye wadau na marafiki walitoa mawazo yao kuwa tuifanye tu hapa hapa maana ni wimbo ambao una mahadhi ya kinyumbani zaidi pia una midundo ya asili ya pwani. Ni wimbo ambao unahitaji uoneshe maudhui ndio tukaona ifanyike Tanga,” aliongeza.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents