Habari
Daraja jipya la Magufuli wilayani Kilombero lang’olewa nati, watu watatu washikiliwa kwa upelelezi
Imearifiwa kuwa zaidi ya Nati 30 za Daraja Jipya la Magufuli Wilayani Kilombero zimeng’olewa huku watu watatu wakishikiliwa kwa upelelezi.
Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Stephen Kebwe ameiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Ulanga na Kilombero kuendelea kuwashikilia watu hao hadi uchunguzi utakapokamilika.
Daraja la Mto Kilombero lilizinduliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli mapema mwezi Mei 2018 na kuitwa Daraja la Magufuli na lina urefu wa mita 300.
Chanzo:ITV