Habari

Daraja jipya la Magufuli wilayani Kilombero lang’olewa nati, watu watatu washikiliwa kwa upelelezi

Imearifiwa kuwa zaidi ya Nati 30 za Daraja Jipya la Magufuli Wilayani Kilombero zimeng’olewa huku watu watatu wakishikiliwa kwa upelelezi.

Daraja la Magufuli

Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Stephen Kebwe ameiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Ulanga na Kilombero kuendelea kuwashikilia watu hao hadi uchunguzi utakapokamilika.

Daraja la Mto Kilombero lilizinduliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli mapema mwezi Mei 2018 na kuitwa Daraja la Magufuli na lina urefu wa mita 300.

Chanzo:ITV

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents