Burudani
Davido asaini msanii mpya ndani ya lebo yake ya DMW
Davido amezidi kutanua himaya ya lebo yake ya Davido Music Worldwide (DMW) kwa kumsaini msanii mpya.
Ijumaa hii muimbaji huyo alifanikiwa kumsaini Yonda Music kupitia lebo yake hiyo ambayo inawasimamia wasanii wengine wawili akiwemo Mayorkun na Dremo.
Baada ya kumalizana na msanii huyo, Davido kupitia mtandao wa Instagram ameandika, “Welcome @yonda_music to DMW !!!!! 2017 BAD BOY BOUTTA BURN IT UP!!! Big up @abbricks (Lazyboy management) .. YONDA ITS YOUR TIME !!.” Tazama picha zaidi hapo chini.