DStv yawasha moto kuelekea AFCON U-17 2019, Sasa ni mwendo wa Inogilee!
Katika kuhakikisha kuwa Tanzania inaendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya kimataifa na Watanzania kushuhudia mubashara timu yao DStv imetangaza rasmi kuwa itarusha mubashara michuano ya kombe la AFCON U17 2019 na hivyo kutangaza kampeni maalum ya kuhamasisha ushindi kwa timu yetu ya Serengeti Boys.
Akizungumza katika hafla ya kuzindua kampeni hiyo ya DStv ijulikanayo kama ‘DStv Inogile’, Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Baraka Shelukindo amesema kuwa katika kuunga mkono kampeni ya kuifanya nchi yetu ifanye vizuri katika michezo mbalimbali, DStv imehakikisha kuwa michuano mbalimbali ya kimataifa inarushwa mubashara tena katika kifurushi cha chini kabisa cha DStv Bomba cha Sh. 19,000 tu – hivyo kuwawezesha mamilioni ya watanzania kuziona timu zetu na hivyo kuongeza ari ya kuziunga mkono kwa hali na mali.
Kwa upande wa michuano ya AFCON ya vijana inayoana mwishoni mwa wiki hii, Shelukindo amesema DStv itakuwa ikifanya kampeni kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa njia ya mitandao na matangazo mbalimbali kuhamasisha na kuitia nguvu timu ya taifa ili iweze kufanya vizuri
“Hili ni swala la kitaifa, hivyo tunataka watanzania popote walipo waweze kushuhudia timu yetu ikipambana kwa ajili ya sifa ya nchi yetu” alisema Shelukindo na kuongeza kuwa DStv inaonekana kote barani Afrika hivyo kitendo cha kuonyesha michuano hiyo ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini kitaufanya ulimwengu kuyashuhudia mashindano hayo na pia kuitangaza nchi yetu. “Kwa michuano hii kuonekana DStv, ina maana kubwa sana kwa nchi yetu, hii ni njia moja wapo pia ya kuitangaza nchi yetu na Afrika na dunia nzima itambue kuwa na sisi tuna uwezo siyo tu wa kuandaa mashindano haya bali pia wa kuyaonyesha”
Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Dr. Omar Singo amesema kuwa kitendo cha DStv kuonyesha mubashara michuano hiyo ni cha kupongezwa kwani ni sifa kubwa kwa nchi yetu. Pia amesema mchango mkubwa unaotolewa na MultiChoice Tanzania katika sekta ya michezo umechangia sana katika kukuza michezo na kuliletea taifa sifa kubwa.
“Serikali inathamini sana michango ya aina mbalimbali inayotolewa na wadau kama DStv katika kukuza michezo hapa nchini. Tunaamini kuwa kwa ushirikiano huu mafanikia haya ambayo tumeanza kuyapata yataendelea na tutafikia azma yetu ya kuwa taifa kubwa kimichezo duniani” alisema Dr. Singo
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake waliowahi kuichezea timu ya Taifa – Taifa Stars ambao walishiriki katika hafla hiyo, mchezaji machachari Amri Kiemba moja kati ya wachezaji nguli waliowahi kuichezea timu ya Taifa ya Tanzania kwa miaka ya nyuma aieleza kuwa , “Kwa mara ya kwanza Tanzania imepewa heshima kubwa kuyaandaa mashindano haya makubwa hivyo ni wajibu wetu sisi watanzania kuonyesha uzalendo na kuwatia moyo vijana wetu ili kuhakikisha wanashinda katika michuano hii na kupata tiketi ya kwenda kwenye mashindano ya dunia nchini Brazil”. Wanasoka wengine nguli walioshiriki katika hafla hiyo ni Fikiri Magoso, Dua Said, Lubigisa Madata, Amri Kiemba, Edibily Lunyamila na Sekilojo Chambua
Mbali ya michuano ya kombe hili la vijana wa chini ya miaka 17 itakayoanza hivi karibuni, wateja wa DStv pia wataendelea kufurahia maudhui mbalimbali zikiwemo sinema na tamthilia mbalimbali kutoka nje na hapa nyumbani kama vile msimu mpya wa vichekesho vya Kitimtim, tamthilia ya HUBA, Rebeca kipindi maarufu cha Shilawadu Xtra na bila kusahau kipindi kipya cha Maisha Yangu kinachoelezea maisha na mapito ya watu mashuhuri kutoka hapa nyumbani Tanzania vyote vikiwa vinapatikana kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo iliyopo katika kifurushi cha Bomba.