Burudani
Dully Sykes awatupia lawama wasanii aliowasaidia kumtosa kwenye show yake ya miaka 15!
Dully Sykes amedai kusikitishwa na kitendo cha baadhi ya wasanii aliowataja kuwa ni ‘wadogo zake’ walioamua kumtosa kwenye show yake ya kuadhimisha miaka 15 ya muziki wake iliyofanyika jana, Escape One.
Akiongea na XXL ya Clouds FM, Dully amesema ameshangaa kuona kuwa wasanii wakongwe wakiwemo Mwana FA, Q-Chief, Chege, Madee, Christian Bella na wengine waliweza kumuunga mkono, lakini wasanii ‘wadogo zake’ kumchinjia baharini.
Msanii huyo mkongwe ambaye pia ni producer, amedai kuwa ni Diamond pekee ndiye aliyemuomba radhi kuwa asingeweza kuwepo kwenye show yake kwakuwa yupo ziarani nchini Rwanda.
Hata hivyo hakuweza kuwataja wasanii hao.