Burudani
Eddy Kenzo ala shavu la ubalozi wa Airtel Uganda
Wiki chache baada ya kuibuka na tuzo ya BET Viewer’s Choice Best New International Artist, kampuni ya Airtel Uganda imemteua Eddy Kenzo kuwa balozi wa kampeni yake mpya, It’s Now.
Eddy Kenzo akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Uganda, Tom Gutjahr
Kampeni hiyo ilizinduliwa na Airtel Africa wiki kadhaa zilizopita ikiwa na lengo na kuibua na kukuza vipaji mbalimbali vikiwemo michezo, muziki na vingine huku ikiwapata watumiaji wake nafasi ya kutumia teknolojia ya mawasiliano ya simu kubaini fursa zinazowazunguka.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Uganda, Tom Gutjahr, Eddy Kenzo ni mfano mzuri wa mtu aliyejikwamua kutoka mtaani na kuwa staa wa muziki si tu nchini mwake bali dunia nzima.