Burudani
Fid Q kuachia video ya ‘Walk it Off’ wikiendi hii
Fareed Kubanda aka Fid Q anatarajia kuvunja ukimya kwa kuachia video ya wimbo wake mpya uitwao ‘Walk it Off’ aliomshirikisha Taz.
Fid Q akitengenezwa vyema nywele zake kabla ya kushoot video hiyo mwishoni mwa mwaka jana
Video ya wimbo huo ilifanyika nchini Afrika Kusini mwishoni mwa mwaka jana. Imeongozwa na Nicroux wa kampuni ya Molotov Cocktail ya Afrika Kusini ambayo miongoni mwa video ilizofanya ni pamoja na Jealousy ya AKA na Rands and Nairas ya Emmy G.
Kupitia Instagram, Fid ameandika: #TANGAZO New visuals by FID Q @therealfidq feat TAZ – directed by @nicroux coming your way this weekend.. Stay tuned.”
Hiyo inakuwa video ya kwanza ya Fid Q kufanya Afrika Kusini.