Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa.
Kushoto ni Ngusa Samike na kulia ni Prof. Godius Kyaharara
Miongoni mwa walioteuliwa ni aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Godius Kyaharara ameteuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa wa Geita.
Aidha aliyewahi kuwa Katibu wa Rais Magufuli Ngusa Samike ambaye alikuwa Katibu Tawala mkoa wa Mwanza amehamishiwa mkoa wa Lindi.