Hii ndio Safu mpya ya Sekretarieti Kuu ya CCM (+ Video)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amempendekeza Daniel Godfrey Chongolo kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.
Chongolo ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar es Salaam, endapo ataidhinishwa na Halmashauri Kuu ya chama hicho, atarithi mikoba ya Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ambaye ni mbunge.
Aidha, Mhe. Samia amempendekeza Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Shaka Hamidu Shaka kuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa chama hicho kuchukua nafasi ya Humphrey Polepole ambaye aliteuliwa kuwa mbunge.
Safu mpya ya Sekretarieti Kuu ya CCM
Katibu Mkuu wa CCM- Ndg Daniel Chongolo (Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Kinondoni)
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM- Ndg Shaka Hamdu Shaka (Anachukua nafasi ya Humphrey Polepole
ambaye ni Mbunge)
Katibu wa Uchumi na Fedha Frank George Hawasi aendelee na nafasi yake
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa
Ngebela Lubinga aendelee na nafasi yake
Katibu wa NEC Oganaizesheni -Ndg Mama Maurdin Kastiko
Ndg Pereira Silima atapangiwa majukumu mengine ya kitaifa)
Naibu Katibu Mkuu Bara-Christina Mndeme (Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma) ndugu Rodrick Mpogolo atapangiwa majukumu mengine ya kitaifa)
Naibu Katibu Mkuu Zanzibar- Abdallah Juma Sadala Mabodi anaendelea na nafasi yake.