Habari
Ikulu yakanusha taarifa ya kumtumbua Balozi wa Tanzania Marekani
Kitengo cha Mawasiliano Ikulu, kupitia kwa Mkurugenzi wake, Gerson Msigwa wameutaka Umma kupuuzia taarifa zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa Rais John Magufuli ametengua nafasi ya Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilson Masilingi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, barua inayosambazwa ni ya kughushi “Fake” na haina ukweli wowote.