Burudani

Irene Uwoya afunguka haya baada ya gazeti moja kudai anamchukia Wema Sepetu

Baada ya gazeti la Ijumaa kutoka na stori “Uwoya: Simpendi Wema” katika ukurasa wake wa mbele, muigizaji wa filamu Irene Uwoya amekanusha madai hayo kupitia ukurasa wake wa instagram.

ijumaa

Pia muigizaji huyo amedai yeye hana tatizo na Wema na sio mtu wa kuwekeana chuki na msanii mwenzake.

Kupitia instagram, Irene aliposti kipande cha gazeti hapo juu na kuandika

“Jamaniii sijawah sema simpend wema… Sina sababu ya kumchukia mim na mpenda kila Mtu na sinaga adui na wala sipend Kuwa na maadui na penda sana kuishi na watu vizuri… Hivo Ndivo nilivyo.”

Pia muigizaji huyo amedai wakati mwingine bifu huanzisha na waandishi wa habari pamoja na mashabiki.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents