Habari

Jeshi la polisi latoa hofu wananchi

Jeshi la polisi nchini limewatoa hofu wananchi mkoani Shinyanga kuwa limeimarisha usalama katika mipaka yote ya mkoa huo ili kudhibiti raia wa kigeni kuingia mkoani humo na kufanya vitendo vya uhalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kikao cha ndani cha askari wa Jeshi hilo, Mkuu wa Jeshi nchini , IGP Simon Sirro amesema vita hiyo inakwenda sambamba na vita ya ugaidi ambapo tayari limeathiri nchi jirani.

“Kwenye mipaka yetu tumejipanga vizuri sana tunafanya operesheni za pamoja na intelijensia za pamoja kwa hiyo hilo sina mashaka nalo, kwa wananchi wa Shinyanga wasiwe na mashaka na hilo kwasababu tumejipanga na tunajua uchaguzi umekaribia pale Kenya ni lazima sisi wenyewe tuimarishe doria zetu mipakani,” alisema IGP Sirro.

“Lazima intelijensia zetu ili anapoingia tuweze kumshughulikia tunajua kuna tatizo la Alshabab kwa wenzetu Kenya kuna suala la ugaidi kwahiyo lazima tuwe makini sana.”

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents