Habari
Jessica Simpson ajifungua mtoto wa pili
Idadi ya wanamuziki maarufu wanaopata watoto inazidi kuongezeka baada ya Kim Kardashian sasa ni zamu ya mwanamuziki Jessica Simpson aliyejifungua mtoto wa Kiume jana (June 30) huko Los Angeles, Marekani.
Huyu ni mtoto wa pili wa Jessica Simpson mwenye (32) pamoja na mpenzi wake Eric Johnson waliyempa jina la Ace Knute Johnson.
Mtoto wa kwanza wa couple hiyo ambaye ni wa kike aitwaye Maxwell, alizaliwa May 1, 2012.
Source: CNN