Burudani
Kanye West amvisha pete ya uchumba Kim Kardashian
Kanye West amemchumbia Kim Kardashian kwenye sherehe binafsi iliyofanyika huko San Francisco, California kwenye uwanja wa AT&T Park.
Rapper huyo anadaiwa kumvisha Kim pete ya almasi iliyotengenezwa na Lorraine Schwartz. Aliukodi uwanja huo na kuwaalika marafiki zake, familia na wengine wa karibu kuhudhuria.
West alialika bendi ya watu wa 50 kupiga live nyimbo kama ya Lana Del Rey, “Young & Beautiful” na wa Keri Hilson, ‘Knock You Down’ ambao naye alishikirishwa akiwa na Ne-Yo.