Habari

Kanye West kumlipa Kim Kardashian $ milioni 1 kila mwaka wakishafunga ndoa

Baada ya Kanye West na mchumba na mama wa mwanaye Kim Kardashian kuweka wazi tarehe ya ndoa yao inayotarajiwa kufungwa May 24, pia hati yao ya makubaliano (Prenup agreement) ambayo wanandoa husaini kabla ya ndoa imesambaa mtandaoni.

kim n kanye w

Katika ‘Prenup’ hiyo ambayo mtandao wa Radar Online wameipata exclusively, moja ya makubaliano waliyoingia wazazi hao wa North West, Kanye atatakiwa kumlipa Kim kiasi cha dola milioni moja kila mwaka katika kipindi chote cha ndoa yao.

Makubaliano mengine ni kuwa pesa zote atakazopata Kim K kupitia reality TV show ya ‘Keeping Up With The Kardashian‘, Clothing Line ya ‘Kardashians’, pamoja na pesa zote anazoingiza kupitia matangazo na promosheni za makampuni, zitaendelea kuwa za kwake (Kim).

Pia Kanye atamwachia Kim K mjengo wao mpya ulioko Bel Air, Los Angeles ambao uko kwenye jina la mkewe Kim.

Hivi ndivyo habari hiyo ilivyoandikwa na Radar.

“The entire process for the prenup for Kim and Kanye has been extremely easy, and relatively drama free. Kanye didn’t even think the couple needed a prenup, and was ready to give Kim carte blanche to all of his financial assets. Yes, he loves Kim that much. There is a huge difference from Kim’s prenup with Kris Humphries….the preparation of their agreement went on several months. It was long and tedious.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents