Burudani
Khadija Kopa kumshirikisha Diamond kufanya remix ya wimbo wa marehemu mwanaye Omary Kopa
Baada ya msanii wa Bongo fleva Nasib Abdul a.k.a Diamond Platnumz kumshirikisha Khadija Kopa kwenye wimbo wake ‘Nasema Nawe’, malkia huyo wa mipasho ana mpango wa kumshirikisha staa huyo kufanya remix ya wimbo wa marehemu mwanaye Omary Kopa.
Kopa amesema kuwa yeye na Diamond wamezungumza na kuweka mipango ya kuurudia wimbo huo uitwao ‘Nipepee Mpenzi Wangu’ uliofanywa na mwanaye, Omary Kopa enzi za uhai wake. Omary alifariki mwaka 2007.
“Mimi na Diamond tumepanga kufanya ‘remix’ ya wimbo huo kwa kuwa mimi naujua vizuri naye anaupenda muda mrefu na amekuwa akiuimba mara kwa mara hivyo tunatumaini tutapata kitu kizuri baada ya kukamilisha kuurekodi wimbo huo,’’ alisema Kopa.
Source: Mtanzania