Habari
Khloe Kardashian adaiwa kumpiga kibuti boyfriend wake French Montana
Baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa miezi nane shemeji wa Kanye West, Khloe Kardashian na boyfriend wake rapper French Montana inasemekana wameachana.
“They are on a break,The relationship got too heavy and Khloe needed to take a step back,” kilisema chanzo kimoja.
US Weekly ambao ndio wa kwanza kuripoti taarifa za kuachana kwao, wamedai kuwa Khloe ndiye aliyempiga kibuti Montana na sababu iliyotolewa ni kuwa rapper huyo alikuwa tegemezi sana kwa Khole, “It grated on her that he became so dependent on her,” kilisema chanzo hicho.