Bongo5 ExclusivesBurudaniHabari

Kinachoendelea Oysterbay Polisi alipo Kizz Daniel, bado yupo ndani

Team ya Bongofive bado ipo hapa kituo cha Polisi cha Oysterbay kujua kinachoendelea baada ya kukamatwa staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Kizz Daniel alasiri ya leo.

Kizz Daniel amekamatwa na waandaaji wa show yake ambayo ilitakiwa kufanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Next Door Arena Masaki Jijini Dar Es Salaam na bado haijawekwa wazi hasa tatizo lilikuwa nini msanii huyo kutotokea jukwaani.

Waandaaji wa Show hiyo Str8upvibe walishaomba msamaha lakini mengi yameongelea kuwa msanii huyo alisahau nguo ingawa uongozi bado hujathibitisha.

Bado yupo ndani kituo cha Polisi na haijajulikana kipi kinaendelea na je atatoka leo au atalala polisi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents