Korea Kaskazini imethibitisha kuwa rais Kim Jong-un ameongoza mwenyewe shughuli ya kufanyia majaribio makombora kadhaa ya masafa ya kadri na yale ya masafa ya mbali. “Makombora kadhaa ya masafa mafupi pia” yalirushwa kutoka rasi ya Hodo hadi bahari ya Japan.
Kwa mujibu wa BBC. Kiongozi huyo alito igizo la kurushwa kwa makombora hayo ili “kuimarisha uwezo wa kujihami” kwa taifa, lilisema tangazo la shirika la kitaifa la habari la nchi hiyo.
Rais wa Marekani Donald Trump aliandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa anaamini Bw. Kim hawezi kuvuruga uhusiano wao pamoja hatua waliyofikia katika harakati za kuleta usalama katika rasi ya Korea.
Aliongeza kuwa Kiongozi huyo wa Korea Kaskazini “anajua kuwa anaweza kunitegemea kwa hilina kwamba katu hatavunja ahadi yake kwangu. Muafaka utapatikan!
“Naamini kuwa Kim Jong-Un fana fahamu fika uwezo wa kiuchumi wa Korea Kaskazini na hatafanya lolote baya kurudisha kudidimiza matumaini hayo,” Bw Trump aliandika katika Twitter yake
Mnamo mwezi Februari mkutano wa Hanoi kati ya Rais wa Marekani, Donald Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ulimalizika bila kufikia makubaliano baada ya Marekani kukataa kutoa nafuu ya vikwazo kwa Korea Kaskazin.
Ripoti yake siku ya Jamapili ya shirika la habari la Korea Kskazini (KCNA) ilisema kuw Bw. Kim amesisitiza umuhimu wa “kulinda ustawi wa kisiasa na kiuchumi” wakati nchi inapokabiliwa na hatari ya kuvamiwa.
Lengo la kufanyia majaribio silaha hizo lilikuwa ni kukagua uwezo wake na jinsi zinavyiofanya kazi ,” ilisema taarifa hiyo.
Rais wa Korea Kaskazini aliwaambia wanajeshi wake kuwa “Amani na Usalama wa hakika unahakikishwa kupitia uwezo wa kujilinda”.
Inaaminiwa hatua ya Korea Kaskazini kufanyia majaribio silaha zake inalenga kuishurutisha Washington kuendeleza mbele mazungumzo ya nyuklia
Mwezi uliyopita, nchi hiyo ilisema kuwa ilifanyia majaribio silaha yake mpya iliyo na uwezo wa ”kuelekeza” makombora katika shambulio maalum.
Hilo lilikuwa zoezi la kwanza tangu kumalizika kwa mkutano wa Hanoi.
Hatua hiyo imepokeleaje?
Katika tarifa ya pamoja wakuu wa usalama nchini Korea Kusini wamethibitisha kuwa Korea Kaskazini “ilirusha makombora ya masafa mafupi kutokarasi yake ya Hodo peninsula karibu na pwani ya mashariki ya Wonsan hadi Kaskazini mashariki
Makombora hayo yalipaa kwa kati ya kilomita 70 hadi 200 kabla ya kuanguka katika bahari ya Japan, waliongeza.
Seoul inasema kuwa iliwahi kuiomba Pyongyang kusitisha shughuli zake kwasababu “itazua hali ya taharuki katika rasi ya Korea”.
“Hatua ya hivi punde ya Korea Kaskazini ni ya uchokozi wakati jamii ya kimataifa inatarajia hatua madhubuti itakayochukuliwa na nchi hiyo kuachana na mpango wake wa nyuklia,” ilisema wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani , kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.
“Tukaribisha azimio la rais Trump kwamba yuko tayari kuendelea mbele na mazungumzo licha ya hatua ya uchokozi wa Korea kaskazini,” ilisema taarifa hiyo.
Bandari ya Hodo iliwahi kutumiwa kufanyia majaribio makombora ya kulipua meli na makombora mengine ya masafa ya mbali.
Mwezi uliyopita Korea Kaskazini ilisema kuwa imefanyia majaribio silaha yenye kombora kali , ikiwa ni mara ya kwanza tangu mazungumzo kati ya rais Donald Trump na Kim Jong un kugonga mwamba.
Kulingana na chombo cha habari cha Korea KCNA jaribio hilo lilisimamiwa na bwana Kim mwenyewe.
KCNA iliripoti kwamba jaribio hilo lilifanywa katika awamu kadhaa za kulirusha , ambapo wachanganuzi wanaamini huenda silaha hiyo ilijaribiwa kutoka katika ardhi, baharini ama angani.
Bwana Kim alisema kuwa hatua hiyo ilikuwa na uzito mkubwa katika kuimarisha jeshi lake.
Ripoti hiyo ilitoa maelezo machache hivyobasi haijulikani iwapo lilikuwa kombora , lakini wadadisi wanasema kuwa huenda ilikuwa silha ya masafa mafupi.
Mwaka uliopita , kiongozi huyo wa Korea alisema kuwa atasitisha majaribio ya silaha za kinyuklia na kwamba hatofanyia majaribio makombora ya masafa marefu huku uwezo wa Kinyuklia wa Pyonyang ukibainika.
Vitendo vya kinyuklia vilionekana vikiendelea, hatahivyo picha za Setlaiti katika kiwanda kikubwa cha kinyuklia cha taifa hilo wiki ilioipita zilionyesha kulikuwa na vitendo vilivyokuwa vikifanyika-zikidai kwamba huenda Korea kaskazini inatengeneza mionzi kuwa mafuta ya bomu.
Taifa hilo linadai kwamba limetenegeza bomu la kinyuklia ambalo linaweza kuingia katika kichwa cha silaha ya masafa marefu pamoja na kombora ambalo linaweza kufika Marekani.