Promotion
Video: Dady Dadyz – Midadi
Hii ni video mpya kutoka kundi la Dady Dadyz Toka jiji la Mbeya ya wimbo wao Midadi.
Ni kundi linaloundwa na jamaa wawili, Solo2 ambaye ni rapper na A2, muimbaji.Kutokana na kuwa na malengo makubwa kwenye muziki wao, mwaka jana walihudhuria tuza Channel O wakiwa kama watazamaji lakini pia kumpa kampani AY. Wakiwa na umri wa mwaka mmoja kwenye muziki, tayari wana nyimbo mbili tu kibindoni, ‘Mzuri’ waliofanya na Lamar na Midadi waliofanya na Mesen Selekta.
Bila shaka Izzo B, Quick Rocka, AY, Neylee na wengine wanaotokea Mbeya City watakuwa wamepata wanajeshi wapya kwenye jeshi lao. Kesho wataachia video ya wimbo wao Midadi.