Burudani

Last Born records ni urithi nitakaouacha hata kwa vizazi vijavyo – Nuh Mziwanda

Nuh Mziwanda amesema label yake, Last Born records si kwaajili yake pekee. Amesema hata siku akiwa ametoweka duniani, itaendelea kuwepo na ndio maana anaendelea kukusanya jeshi.

“Nataka nikizeeka au nikiwa sipo duniani basi niwe nimeacha watu wa kunikumbuka au vitu ambavyo vitakuwa kwenye historia ya maisha yangu, that’s why hivi sasa kwenye studio yangu Last Born records Nina wasanii wawili wapya kabisa ambao ntawatambulisha baada ya miezi miwili au mitatu ijayo,” amesema muimbaji huyo.

“Mmoja anaitwa Chichi Chadala, huyu yeye anaimba muziki wa kurap na mwingine anaitwa Computer, huyu yeye anaimba na huyu computer ndiye kaandika wimbo wangu wa Anameremeta, “ Mziwanda alikiambia kipindi cha VMix cha Channel 10.

Imeandikwa na Nelson Munema

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents