Habari

Mabadiliko Baraza la Mawaziri, Dkt. Kigwangalla ala shavu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya mabadiliko katika Baraza lake Mawaziri ambapo baadhi ya mawaziri wamepoteza nafasi zao huku baadhi wakipanda na wengine wapya wakiteuliwa.

Akitangaza mabadiliko hayo leo Ikulu jijini Dar es salaam, Rais Magufuli wizara zimeongezeka kutoka 19 za awali hadi kufikia 21.

Naibu waziri wa Nishati, Mh Medard Kalemani ameteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo amebaki Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ameteuliwa kuwa Juliana Shonza.

Waziri wa Utalii, amekuwa aliekuwa Wizara afya, Dk Hamisi Kingwangala, na Nibu wake Kasunda, Wizara na Mambo ya Nje, Agustino Mahiga na Naibu atakuwa Suzan Kolimba, Viwaza ya viwanda na biashara, Charles Mwijage na Naibu wake Mhandisi Stella Manyanya, Waziri wa Madini Angella Kairuki,Mh. Charles Tizeba anabaki kuwa Waziri wa Kilimo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents