Burudani
Malaika amtaja mwanaume spesho kwenye maisha yake
Malaika ni msichana mrembo ambayo macho ya wanaume wengi yanamtamani lakini yupo mtu mmoja muhimu zaidi aliyeushikilia moyo wake.
Mtu huyo kwa mujibu wa Malaika, ndiye anayefanya kila kitu katika muziki wake.
“Nipo na mtu, best yangu, baada ya mama na yeye pia,” Malaika alikiambia kipindi cha Chill na Sky hivi karibuni.
“Ananisupport kwa kila kitu, kila kitu ambacho unakiona Malaika anakifanya na yeye pia.”
Amesema ndiye mtu anayeishi naye kwa sasa huku uhusiano wao ukiwa ni wa miaka minne.
Mfahamu zaidi Malaika kwa kusikiliza kipindi cha Chill na Sky hapo chini.