Habari

Mama ajifungua watoto watano kwa mpigo Somalia

Mwanamke mmoja jijini Mogadishu, Somalia amejifungua watoto watano kwa mpigo. Mama na watoto wake wote wanaendelea vizuri japo bado wamelazwa kwa uangalizi zaid wa afya zao.

Taarifa za tukio hilo la nadra zimetolewa na hospitali moja jijini humo ambapo watoto hao wamezaliwa.

Taarifa juu ya utambuliso wa mama na jinsia za watoto hao bado hazijawekwa wazi. BBC inafuatilia taarifa hii na tutakujuza zaidi katika taarifa zetu zijazo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents