Mama ajifungua watoto watano kwa mpigo Somalia
Mwanamke mmoja jijini Mogadishu, Somalia amejifungua watoto watano kwa mpigo. Mama na watoto wake wote wanaendelea vizuri japo bado wamelazwa kwa uangalizi zaid wa afya zao.
Taarifa za tukio hilo la nadra zimetolewa na hospitali moja jijini humo ambapo watoto hao wamezaliwa.
Taarifa juu ya utambuliso wa mama na jinsia za watoto hao bado hazijawekwa wazi. BBC inafuatilia taarifa hii na tutakujuza zaidi katika taarifa zetu zijazo.
A mom gave birth 5 little babies (quintuplets) in our hospital, one of the rarest births in the world. The Mom and her babies are healthy and now monitored by our doctors. Thanks to our health professionals who made this possible. pic.twitter.com/gkMeGGUmke
— Mogadişu Somali Türkiye Recep Tayyip Erdoğan EAH (@MSTH2014) August 3, 2020