Michezo
Matokea ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya
Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya iliendelea usiku wa March 9,kwa michezo miwili kupigwa barani Ulaya. Klabu ya Chelsea ilikuwa mwenyeji wa klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa, wakati Zenit walicheza dhidi ya Benfica.
Timu ya Chelsea ilitolewa baada ya kufungwa 2-1 na Paris Saint Germain kwenye uwanja wa Stamford Bridge, Benfica wao walishinda 2-1 dhidi ya Zenit
Mabingwa hao wa Ufaransa walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 16 kupitia kwa Adrien Rabiot lakini Chelsea wakazawazisha dakika 11 baaade mfungaji akiwa ni Diego Costa. Zlatan Ibrahimovic akamaliza shughuli kwa kuifungia PSG bao la ushindi dakika ya 67 kufuatia krosi tamu ya Angel di Maria.