Habari

Miaka 60 ya Uhuru Wizara ya Maliasili na Utalii kukutana kileleni

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas  Ndumbaro, amewataka watanzania kujitokeza kupanda mlima Kilimanjaro katika kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro

Hata hivyo Waziri Ndumbaro ameongeza kuwa wizara hiyo imeazimia kupanda kilele cha Mlima Kilimanjaro na watanzania 300 na mpaka sasa waliojisajili ni zaidi ya 120 .

Aidha Waziri huyo mwenye dhamana ameongeza kuwa gharama za upandaji Mlima zimepunguzwa hivyo mtanzania mmoja atalipia shiling laji 8 ambazo zitakidhi huduma zote muhimu kwa siku sita.

Mbali na hayo Waziri Ndumbaro amewaomba watanzania kuwa mabalozi wa mlima Kilimanjaro huku akisisitiza kuwa mlima huo mrefu haupo Afrika bali ni barani Afrika nchini Tanzania

BY: Fatuma Muna

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents