Mr. Nice na Harmonize wapigana vikumbo Rwanda (video+picha)
Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Mr. Nice jana usiku amefanya show ya babu kubwa nchini Rwanda kwenye tamasha la Seka Fest lililohudhuriwa na mastaa kibao akiwemo Idris Sultan, Erick Omondi na Miss Rwanda mwaka 2018, Liliane Iradukunda.
Show hiyo iliyojaza ukumbi mkubwa wa burudani nchini Rwanda wa Camp Kigali, ulijawa na shangwe za makelele mkali huyo wa TAKEU alivyoanza kutumbuiza jukwaani.
Show hiyo ambayo ni moja kati ya matamasha makubwa nchini Rwanda ambalo hufanywa mara moja kwa mwaka limefanyika masaa machache baada ya msanii mwingine kutoka Tanzania, Harmonize ambaye naye alikonga nyoyo za mashabiki nchini humo kwa kupiga show ya kibabe.
Hali hiyo imeleta mfananisho wa show zote mbili ambapo bila ubishi show zote mbili zilipiga nyomi.
Tazama picha za show ya jana aliyotumbuiza Mr. Nice nchini Rwanda.
Photos by inyarwanda.rw