Msondo Ngoma na ujio wa Album mpya mjini, mashabiki watakiwa kukaa mkao wa kula.
Msanii wa Band ya Msondo Ngoma Rajabu Said @rijo_voice amewataka watanzania kukaa mkao wa kula kupokea ujio wa album mpya kutoka kwa wakongwe hao wa muziki Afrika.
@rijo_voice ameyasema hayo wakati wa mahojiano na Bongo5 Media alipokuwa akitambulisha wimbo mpya wa Veronica ambao utapatikana kwenye album hiyo.
@msondo_ngoma_ ni miongoni mwa Band kongwe nchini huku Mkuu wa kitengo cha Teknolojia, Nicolas Clavel akielezea namna wanavyofanya jitihada za kuifanya band hiyo kwendana na wakati uliyopo.