Burudani

Mtabiri abaini mambo mazito kwenye maisha ya Lady Jaydee mwaka huu

Kwa Lady Jaydee, mwaka 2015 utakuwa wenye mafanikio makubwa, ndoa mpya, stress kiasi na magonjwa lukuki, kwa mujibu wa mtabiri!

jaydee

Mtabiri huyo alialikwa na Lady Jaydee kwenye kipindi chake, Diary ya Lady Jaydee ambapo alidai kuwa mwaka huu muimbaji huyo atapata pesa nyingi kupitia muziki wake lakini kiafya akitabiriwa homa nyingi na kukifiria kifo mara kwa mara.

“Kuna vitu vitaisha mwaka huu ambavyo itabidi uache,” mtabiri huyo alimweleza Jide. “KAwanza hii ni possibility you need to avoid, kuna wakati hali ya kifo itakupa stress sana, unaweza ukasema maisha yangu yatakuaje?

“Usifikirie hivyo, utakuwa unafikiria kifo, utafikiria baada ya kifo nini kinaendelea, utakuwa unafikiria siku nikifa nitaenda peponi au nitaenda motoni, kwahiyo kifo kitakuja kwako lakini usifikirie, kwamba ukiumwa tu kidogo haa nitakufa, no hufi, because ningeona kifo kwenye utabiri wako wa mwaka 2015! Mwaka huu utaumwa kidogo, utaumwa magonjwa, afya yako itakuwa weak sana, kama ungeolewa ingekuwa kama kinga ya kwa mwaka huu, lakini mwaka huu utakuwa na furaha sana kwa sababu ya pesa, kwahiyo kama utakuwa na pesa basi utaishi muda mrefu.

Pia alitabiriwa kufanya vizuri kimuziki ndani ya mwaka 2015-2016 na pia kuolewa na mwanaume maarufu na tajiri.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents